*Pata habari zote za hapa mjini Dodoma (Capital City) na nyinginezo kutoka MIJI mbalimbali hapa Tanzania na nje ya Tanzania* >>>>>>> *Pata habari zote za hapa mjini Dodoma (Capital City) na nyinginezo kutoka MIJI mbalimbali hapa Tanzania na nje ya Tanzania*

  • Wednesday, 8 April 2015

    Tanzania yapangwa kwenye kundi gumu Afcon 2017.

    stars-1111111-FILEminimizer
    Michuano ya kombe la mataifa ya Afrika kwa mwaka 2017 imepangiwa makundi yake ya michuano ya kufuzu hii leo (jumatano) huko Cairo nchini Misri kwenye makao makuu ya shirikisho la soka barani Afrika CAF .
    Makundi hayo yaneshuhudia timu kubwa zikipangwa kwenye nafasi za kwanza huku zikipangwa na mataifa madogo kama ulivyo utaratibu wa kugawa nafasi kuendana na viwango vya ubora.
    Timu ya taifa ya Tanzania imepangwa kwenye Kundi G ambako inaambatana na timu za taifa za Misri , Nigeria na Chad .
    Makundi hayo ni kama ifuatavyo.
    Kundi A ; Tunisia , Togo , Liberia , Djibouti . Kundi B ; Congo Drc , Angola , CAR , Madagascar.
    Kundi C Mali , Equatorial Guinea , Benin , South Sudan. Kundi D; Burkina Faso ,Uganda , Botswana , Comoros.
    Kundi E; Zambia , Congo , Kenya , Guinea-Bissau. Kundi F ; Cape Verde , Morocco , Libya, Sao Tome.
    Kundi G; Nigeria , Egypt , Tanzania , Chad. Kundi H; Ghana , Mozambique , Rwanda , Mauritius.
    Kundi I ; Ivory Coast , Sudan , Sierra Leone , Gabon . Kundi J; Algeria , Ethiopia , Lesotho , Seychelles.
    Kundi K ; Senegal , Niger , Namibia , Burundi . Kundi L ; Guinea , Malawi , Zimbabwe , Swaziland.
    Kundi M ; Cameroon , South Africa , Gambia , Mauritania .
    Michezo ya kufuzu kwa makundi haya itaanza kupigwa mwezi juni mwaka huu ikiendelea mpaka mwakani .

    0 comments:

    Post a Comment