*Pata habari zote za hapa mjini Dodoma (Capital City) na nyinginezo kutoka MIJI mbalimbali hapa Tanzania na nje ya Tanzania* >>>>>>> *Pata habari zote za hapa mjini Dodoma (Capital City) na nyinginezo kutoka MIJI mbalimbali hapa Tanzania na nje ya Tanzania*

  • Thursday, 8 January 2015

    Mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates kwenye huu mradi wa maji unaotokana na taka(Kinyesi) cha binadamu!


    billsMmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates amekunywa maji yaliotengenezwa kutokana na kinyesi cha binaadamu kama maonyesho ya teknolojia mpya itakayoweza kutoa maji safi katika Mataifa yanayoendelea.Mwanzilishi huyo wa kampuni ya Microsoft amesema kuwa ataisambaza mitambo ya teknolojia hiyo mpya kote duniani baada ya kuifanyia majaribio na kuridhika nayo mwishoni mwa mwaka huu.Teknolojia hiyo imeungwa mkono na shirika la WaterAid ambalo limesema kuwa litasaidia sana katika maeneo ya mengi ya miji.Kulingana na shirika hilo takriban watu millioni 748 hawana maji safi ya kunywa.Katika kanda ya video iliyowekwa katika blogu yake,Bill Gates alishuhudia kinyesi cha Binaadamu kikiingizwa katika mtambo huo kabla ya kunywa maji yaliokuwa yakitoka baada ya kuboreshwa ambapo huchukua dakika tano kukamilika.

    0 comments:

    Post a Comment